‘Mastaa’ wafurahishwa na alichofanya Tessy kwa Aslay

‘Mastaa’ wafurahishwa na alichofanya Tessy kwa Aslay

Tessy ambaye ni mama mtoto wa msanii Aslay, amepongezwa na ma-star mbalimbali baada kuonesha  ‘kumsapoti’ Aslay kufuatia na show yake inayotarajia kufanyika Septemba 30, ya kuadhimisha miaka 10 katika tasnia ya uimbaji.

Ambapo Tessy ametengeneza video akiwa na mtoto wake Mozza aliyezaa na Aslay akiwataka mashabiki kununua ‘tiketi’ za shirikiki kwenye show hiyo ya Aslay.

Mastaa mbalimbali wameoneshwa kuvutiwa na kitendo hicho huku baadhi yao wakidai kuwa wawili hao ambao inafahamika waliachana miaka mingi iliyopita, waweze kurudiana.

Kati ya ma-star hao ni Nandy amedai kuwa amefurahishwa na kitendo hicho, huku kwa upande wa Dulla Makabila yeye amefurahishwa kwa kitendo alichofanya Tessy na kuwashauri wawili hao waweze kurudiana.
.
.
.
#MwananchiScoop
#BurudikaNasi






Comments 0


Leave a Reply

Author

Hello, I'm
Aisha Lungato

A digital journalist and writer for Mwananchi Scoop. My stories are around entertainment, lifestyle, artist profiles and career.


Latest Post